Jumapili, 12 Mei 2013

KUJITANGAZIA UHURU
Kujitangazia uhuru kutoka katika utumwa wa kiroho, kuwatangazia nduguzako uhuru kutoka katika utumwa wa kiroho ni kazi inayohitaji kusimama kwako mwenyewe na kujitambua.
Ezekiel 37:3    BWANA MUNGU alimwambia Ezekieli "Mwanadamu, je mifupa hii yaweza kuishi?"  Ezekiel akamjibu "BWANA MUNGU wajua wewe"

 Ezekiel 37:4  akamwambia "Toa unabii juu ya mifupa hii uiambie enyi mifupa mikavu lisikie neno la  BWANA"

Ezekiel 37:5  BWANA MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya "Tazama nitatia pumzi ndani yenu nanyi  mutaishi.

Kama BWANA MUNGU alivyomwambia Ezekieli, na wewe ni Ezekieli wa familia yako, biashara yako, mashamba yako, ndoto zako na nchi yako. Tabiri kwa yale unayotaka yatokee ondoa ukaufu, tabiri uzima.
Ondoa kushindwa, tabiri ushindi ndipo utayaona mafanikio makubwa.

Ezekiel 37:11    Kisha akamwambia Ezekieli "Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli, tazama wao husema mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea, tumekatiliwa mbali kabisa.

Ezekieli 37:12-13  BWANA MUNGU akamwambia ezekieli "Basi tabiri uwaambie BWANA MUNGU asema hivi, tazama nitafunua makaburi yenu na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu enyi watu wangu, nami nitawaingiza katika nchi yenu.
 
Kuna ushindi baada ya kuwekwa huru, kuna kutawala baada ya kuwekwa huru, kuna umiliki baada ya kuwekwa huru, kuna amani baada ya kuwekwa huru.
Chukua hatua leo ukajitangazie uhuru wako na ubarikiwe na BWANA kwa kujitangazia uhuru wako.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni