Jumapili, 12 Mei 2013

                HALELUYA MWANA WA MUNGU



   SOMO LA LEO: usemi wa mwanadamu.

 usemi wa mwanadamu ni uwezo wa mwanadamu wenye nguvu zaidi. kwa sababu kwa manenoyake anaweza kuleta manufaa makubwa. lakini pia anaweza kuleta hasara kubwa katika neno la MUNGU bibilia inasema katika (MITHALI 12:18) kuna anenaye bila kufikili, kama kuchoma kwa upanga bali ulimi wa mwenye haki ni afya

Matatizo mengi uliyo nayo katika maisha yako, ndoa, biashala,kazini, shambani, na katika jamii anayo kuzunguka. yanasababishwa na matumizi mabaya ya usemi wako unawakwaza watu kwa usemi wako,

(MITHALI 10;19) katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu baliu yeye azuiaye midomo yake hufanya akili, tunza mdomo wako kwa usalama wako mwenyewe, Wasifu wa mtu sio mavazi tu bali hutemea maneno ya kinywa chako mwenyewe

Mpumbavu na mwenye hekima wakinyamaza huwezi kuwatambua mpumbavu ni yupi na mwenye hekima ni yupi, utawatambua tu wakianza kujieleza ndipo atajulikana mpumbavu na mwenye hekima, jitaidi sana kufikili kabla haujasema usije ukaonekana mpumbavu machoni pa watu,

hiki ndicho kipimo cha utu wako na heshima yako mbele ya wanao kutazama, ni aibu kwa mtu mwenye utashi na ukwasi kutamka hadhalani maneno yasiyo faa mbele ya jamii

BWANA YESU AKUBALIKI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni