Jumapili, 12 Mei 2013

BWANA WETU YESU ASIFIWE

   SOMO LA LEO: Kuwa  kiungo katika mwili wa christo yesu


  ukristo sio dini bali usiano na bwana wetu yesu. kwa yesu wetu hakuna dini. na watu hawaendi mbinguni kwa tiketi ya  madhehe yao, hutaingia mbinguni kwa upentecoste au uassembles wako.

Ndugu yangu. kuwa na majina makubwa ya madhehebu hakukusaidii kitu. Bali kinacho saidia ni ushirika wako na bwana wetu yesu.  neno  la BWANA linasema hivi katika kitabu cha WAEESO5;29-30 maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama kristo naye anavyolitendea kanisa.sio dhehebu wala dini.

kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. yani kristo. kwanini leo kuna kutengana baina ya madhehebu, sote tu viungo vya mwili wake yesu,mbinguni tutaingia kwa utakatifu tu wala sii vinginevyo bwana akusaidie uponyeke imani yako


kumbuka kuwa sehemu ya mwili  kuna faida tano

1. KUPENDWA hakuna mtu alie wai kuchukia kiungo cha mwili wake mwenyewe .unapendwa na yesu kwa sababu uu kiungo cha mwili wake
2.KULINDWA hakuna mtu asie linda viungo vyo mwili wake. kristo naye utulinda
3.KUWEZESHWA hakuna asie viwezesha viungo vya mwili wake, una wezeshwa na yesu kwasababu uu sehemu ya mwili wake yani kanisa
4.KULISHWA. unalishwa na yesu kwasababu wewe ni sehemu ya nwili wake (kanisa)
5.KUJALIWA. hakuna asie ujali mwili wake bali uulisha na kuutunza kama yesu anavyo litendea kanisa lake hapa Duniani


                                         UBARIKIWE NA BWANA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni